VIJANA
wawili wenye asili ya kiasia, wakazi wa jiji la Arusha, wametiwa
mbaroni na polisi mkoani hapa kwa tuhuma ya kukutwa na kete 170 za dawa
za kulevya aina ya heroin na bangi kete 300.
Walihifadhi
dawa hizo kwenye mfuko mweusi aina ya sandarusi na zingine kete 170
zikiwekwa kwenye mpira wa kiume (kondomu) ndani ya gari.
Kamanda
wa Polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni
Mavan Tapel (20) na Nisha Patel (26), wote wakazi wa nyumba za Shirika
la Nyumba (NHC) eneo la Metropole jijini Arusha.
Sabas
alidai vijana hao walikutwa na misokoto 300 ya bangi, kete 170 za
heroin zilizokuwa kwenye mfuko wa sandarusi na kete 150, zilizowekwa
kwenye kondomu ya kiume.
Alisema watuhumiwa hao, walikuwa wakitumia gari aina ya Nissan Primera, ambalo lilitumika kuhifadhi dawa hizo za kulevya.
Watuhumiwa
bado wanaendelea kuhojiwa katika kituo cha polisi jijini hapa, kutokana
na upelelezi wa tukio hilo kutokamilika. Hata hivyo, alisema thamani ya
dawa hizo, hazikuweza kufahamika mara moja.
>>Habari leo
>>Habari leo
0 comments:
Post a Comment