pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Ripoti ya Israel juu kushindwa katika vita vya Gaza

Ripoti juu ya kushindwa Israel katika vita vya Gaza
Mashirika ya usalama ya Israel yametoa ripoti na kueleza kuwa sababu kuu iliyolilifanya jeshi la utawala huo kushindwa katika vita ilivyoanzisha huko Ghaza ni taarifa zisizo sahihi na kushindwa kukabiliana na muqawama wa Palestina. mashirika ya usalama ya utawala wa Kizayuni likiwemo shirika la taarifa za ndani la Israel(Shabak) na shirika la taarifa za kijeshi (Aman) yamechapisha ripoti na kufichua kuwa, jeshi la Israel  liligonga mwamba katika kupata taarifa yoyote kuhusu mahali walipo makamanda wa muqawama wa Palestina na hata viongozi wa kisiasa wa Palestina huko Ghaza.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo,mashambulizi ya Israel huko Ghaza  hayakuzaa matunda kwa mujibu wa viwango vyote vya kijeshi au kiitelijinsia na kwamba vita hivyo vimeonyesha kuwa utawala wa Kizayuni hauna taarifa za kweli kuhusu matukio ya Ghaza.

0 comments:

Post a Comment