pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Kikwete amtumia salamu za pongezi Rais wa Iran

Kikwete amtumia salamu za pongezi Rais wa Iran
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemtumia salamu za pongezi Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mnasaba wa maadhimisho ya miaka 36 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu. Katika ujumbe wake huo, Rais Jakaya Kikwete amempongeza Rais Rouhani na taifa la Iran kwa ujumla kwa mnasaba wa maadhimisho ya miaka 36 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu yaliyofikia kilele hapo jana. Ujumbe huo uliotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Tanzania umemnukuu Rais Kikwete akiitakia kila la kheri Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika maadhimisho ya mwaka wa 36 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu yaliyotokea mwaka 1979 kwa uongozi wa Imam Ruhullah Khomeini (M.A).
Rais Kikwete amesisitiza katika salamu zake hizo za pongezi kwamba, Tanzania na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zina uhusiano mkongwe, wa kihistoria na wa kiutamaduni. Amesema Dar es Salaam na Tehran zina ushirikiano mzuri katika nyuga mbalimbali na kwamba, ana matumaini nchi mbili hizi zitapanua zaidi ushirikiano wao katika sekta nyingine kama za usafiri, biashara, uwekezaji, teknolojia, mafuta, gesi na mawasiliano. Ikumbukwe kuwa, jana ilikuwa kilele cha maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu hapa Iran, ambapo mamilioni ya wananchi waliandamana na kutangaza tena himaya na uungaji mkono wao kwa Mapinduzi ya Kiislamu na mfumo wa Kiislamu unaotawala hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment