pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Edward Lowassa: Nimeshawishika kuwania urais TZ

Edward Lowassa: Nimeshawishika kuwania urais TZ
Hatimaye mbunge wa Monduli nchini Tanzania, Edward Lowassa, amesema ameshawishika kugombea urais wa nchi hiyo kwa tiketi ya chama cha CCM na ametangaza rasmi kuwa, atachukua fomu ya kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho tawala. Lowassa ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Nne huko Tanzania, kwa muda mrefu amekuwa akitajwa kuwa mmoja wa makada wa CCM wenye nia ya kugomea urais, lakini hakuwahi kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo. Lakini jana, alizungumzia suala la urais ambalo lilimfanya yeye na wenzake watano wafungiwe kwa kipindi cha miezi 12 kujihusisha na harakati hizo baada ya Kamati Kuu ya CCM kuwatia hatiani kuwa walianza kampeni mapema kabla ya muda kufika. "Nimepata barua za ushawishi kutoka kwa watu wengi, lakini nyinyi nimeshawishika," alisema Lowassa nyumbani kwake mjini Dodoma wakati alipokuwa anazungumza na masheikh wa misikiti ya Wilaya ya Bagamoyo wanaokadiriwa kufikia 50 ambao pia walikwenda mjini humo kwa ajili ya kumshawishi aingie kwenye kinyang'anyiro cha urais na kumkabidhi mchango wa Sh700,000 kwa ajili ya kuchukulia fomu.

0 comments:

Post a Comment