pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Kamishna Msaidizi wa Polisi afariki dunia

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema.
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Shabani Kimea (54), amefariki dunia katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu.
 
Taarifa iliyotolewa na kuthibitishwa na Msemaji wa Polisi, Advera Senso, imesema Kimea alifariki juzi na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na familia ya marehemu imesafirisha mwili wa marehemu kwenda kijijini kwao Mwera mkoani Tanga, kwa mazishi.
 
Senso alisema Jeshi la Polisi limepata pengo kubwa kwa kuondokewa na kamishina huyo kwa kuwa alikuwa mtendaji hodari hali iliyomfanya kutunukiwa nishani ya utumishi wa muda mrefu na Rais Jakaya  Kikwete.
 
Alisema Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema amezipokea taarifa za kifo hicho kwa huzuni hasa ikizingatiwa hivi sasa askari mmoja anahudumia watu takribani 1300 hadi 1500. 
 
ACP Kimea alijiunga na Jeshi la Polisi Mwaka 1985 na kupandishwa vyeo mbalimbali hadi kufikia cheo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi ambapo mpaka mauti yanamkuta alikuwa mkuu wa Kitengo cha Mipango ya Raslimaliwatu, Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na nafasi nyingine alizowahi kushika ni pamoja na kuwa Mkuu wa Upelelezi wilayani Misungwi, Mkuu wa Polisi wilayani Misungwi na Geita pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Polisi mkoani Morogoro.
chanzo Nipashe

0 comments:

Post a Comment