pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Kuunganishwa umeme kutarejea wiki mbili zijazo

Meneja Uhusianio wa Tanesco, Badra Msoud.
Wakati huduma za kuunganishia umeme wateja wapya zikiwa zimesimama tangu mwishoni mwa mwaka jana kutokana na uhaba wa nguzo, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema huduma hiyo itarejea kama kawaida baada ya wiki mbili.
 
Baadhi ya wananchi wameeleza kuwa pamoja na makao makuu ya shirika hilo kueleza nguzo hakuna, lakini wapo wateja wengine hupatiwa nguzo kwa njia zisizo halali.
 
Akizungumza na gazeti hili, Meneja Uhusianio wa Tanesco, Badra Msoud, alisema upo uhaba mkubwa wa nguzo za umeme na kwamba zilizopo ni kwa ajili ya dharura.
“Wateja wetu wasubiri kwa wiki mbili, kwani nguzo hizo ziko njiani kutoka South Africa na nyingine zinatoka hapahapa nchini,” alisema.
 
Kampuni za ndani zilizoshinda zabuni ya kusambaza nguzo za Tanesco ni Critical Engineering Solutions Construction Co, Sao Hill Industries Ltd na Mufindi Wood Poles.
Kampuni za nje ni kutoka Afrika Kusini za Treated Timbers Products, Low’s Treated Timbers (Ptg), Rousant International  na Maghilika Timber Ptg Ltd.
 
Badra alisema kuwa Tanesco inatumia sheria ya manunuzi na kwamba kampuni zote zilishindanishwa kwa tenda na zilizoshinda zilitimiza vigezo ikiwa ni pamoja na bei elekezi.
 
Kwa mujibu wa Badra, kabla ya nguzo kupokelewa na Tanesco, hufanyiwa uchunguzi wa kina ikiwa ni pamoja na majaribio ya kiufundi ili kuthibitisha ubora na kama zinakidhi viwango vya ubora vilivyoainishwa kwenye zabuni ndipo hati za kuzipokea zinasainiwa.
chanzo Nipashe

0 comments:

Post a Comment