pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

ARSENAL YACHOMOLEWA UEFA, DIEGO COSTA AIZAMISHA AC MILAN

KLABU ya Arsenal imeaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya sare ya 1-1 na mabingwa watetezi usiku huu Uwanja wa Allianz Arena mjini Munich.
Timu ya Arsene Wenger iliyofungwa mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza Uwanja wa Emirates sasa inahamia kwenye Europa League baada ya kipigo ha jumla cha mabao 3-1.
Bastian Schweinsteiger alitangulia kuifungia Bayern dakika ya 54 na Lukas Podolski akaisawazishia Arsenal dakika ya 57.


Tumble: Oxlade-Chamberlain is brought down again, this time by Bastian Schweinsteiger
Oxlade-Chamberlain akienda chini baada ya kukutana na Bastian Schweinsteiger
Surrounded: Ribery battles for the ball with Oxlade-Chamberlain (right) and Cazorla (left)Frank Ribery akiwatoka Oxlade-Chamberlain (kulia) na Santi Cazorla (kushoto)
  Wachezaji wa Bayern  wakisherehekea baada ya kuitoa Arsenal





MADRID


AC MILAN imeungana na Arsenal kuipa mkono wa kwaheri michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kutandikwa mabao 4-1 na Atletico Madrid usiku huu Uwanja wa Vicente Calderon katika mchezo wa marudiano Hatua ya 16 Bora.
Milan sasa inaaga kwa kipigo cha jumla cha 5-1, baada ya awali kufungwa 1-0 nyumbani. Diego Costa alitangulia kuifungia Atletico dakika ya tatu pasi ya Koke, kabla ya Ricardo Kaka kuisawazishia Milan dakika ya 27 pasi ya Poli.
Milan ikatepeta na kuongezwa mabao matatu wafungaji Turan dakika ya 40, pasi ya Raul Garcia, aliyefunga la tatu dakika ya 71 kwa pasi ya Gabi na Diego Costa akakamilisha safari ya Atletico kuelekea Nane Bora ya Ligi ya Mabingwa kwa bao zuri dakika ya 85 pasi ya Sosa.

Diego costa katika harakati za kufunga goli

0 comments:

Post a Comment