pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Mamba mla watu auawa Morogoro

Morogoro. Mkazi wa Kijiji cha Bwakila Chini, Kata ya Bwakila Chini, Maloda Sitini amefariki dunia baada ya kuliwa na mamba tukio lililotokea katikati ya mwezi uliopita katika Mto Mgeta, Wilaya ya Morogoro.
Diwani wa Kata ya Bwakila Chini, Mohamed Pesa alisema kuwa marehemu alifikwa na kifo wakati akivuka Mto Mgeta, Februari 13 mwaka huu na ghafla alikamatwa na mamba huyo aliyemshambulia sehemu mbalimbali za mwili na baada ya kumzidi nguvu, alimzamisha majini kisha kumwua na kumla.
Pesa alisema kuwa ndugu wa karibu wa marehemu walimtafuta Sitini kwa siku 18 bila mafanikio na walitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na kata hiyo.
Alisema kuwa uongozi wa kijiji ulibaini kaliwa na mamba baada ya kuona mabaki ya vipande vya nguo alizokuwa amevaa marehemu na ndipo ukawekwa mtego wa kumnasa mamba huyo. Diwani huyo alisema kuwa mamba huyo alinaswa Machi 2 saa 4 usiku.
“Katika kata yangu kuna tukio la mamba mla watu kauawa na mpango wa kumuua ulitimizwa baada ya kufahamika kuwa mtu mmoja aliyetambulikwa kwa jina la Maloda Sitibi kufariki dunia kwa kuliwa na mamba.
"Kwa bahati mzuri, ushirikiano wa uongozi wa Taasisi ya Jukumu ya Society na wananchi walifanikiwa kumwuua kwa kutega mtego uliowezesha kumnasa mamba huyo," alisema Pesa.
Pesa alisema baada ya kuuwawa, mamba huyo alipasuliwa na tumboni mwake alikutwa na mifupa mbalimbali ya binadamu, nywele za kichwani na bangili.
Baba mzazi wa marehemu, Mzee Sitibi alichukua mabaki hayo ya mifupa ya mwanawe na kwenda kuyazika.
Diwani huyo alitoa wito kwa wakazi wa kata hizo wananchi wanapaswa kuchukua tahadhali kubwa wakati wanakaribia ama kuvuka mito mikubwa inayopita katika kata hiyo hasa kipindi hiki cha mvua za masika.

Mwananchi

0 comments:

Post a Comment