Wizara
 ya Fedha kupitia Naibu wake Waziri wa fedha Mh. Mwigulu Nchemba 
wametangaza uamuzi wa kufuta malipo ya Wabunge waliosusia vikao vya 
mchakato wa Katiba vinavyoendelea Dodoma.
Uamuzi huu umetangazwa ikiwa ni siku ya pili tangu Wajumbe wa Bunge 
la Katiba Kutoka UKAWA wasusie Shughuli za Bunge la Katiba kwa Madai 
wamechoka matusi na Kuburuzwa kwenye Bunge hilo.
Hii leo Naibu waziri wa Fedha Mh.Mwigulu Nchemba ambaye kwa Sasa 
anakaimu Kuwa Waziri wa Fedha tangu April 10  20014 baada ya  Waziri wa 
Fedha kupata safari ya kikazi nchini Marekani,amefuta Malipo ya wabunge 
waliosusia Mchakato huo wa Katiba.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ameagiza Benki zote kurudisha Cheque za 
Malipo ya Posho na seating allowance ambazo zilipelekwa Bungeni April 16
 ili ziwekwe kwenye akaunti binafsi za Wabunge ikiwa ni Malipo ya Mpaka 
April 30.






 

0 comments:
Post a Comment