pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Real Madrid yairarua Beyern

Real madrid yafuzu kwa fainali ya kombe la mabingwa bara Uropa
Shujaa wa Real alikuwa ni Sergio Ramos aliyefunga mabao mawili, la kwanza dakika ya 16 pasi ya Luka Modric na la pili dakika ya 20 pasi ya Pepe kabla ya Mwanasoka wa Bora Dunia, Cristiano Ronaldo kumaliza kazi kwa kufunga mabao mawili dakika ya 34 pasi ya Gareth Bale na dakika ya 90.
Kipindi cha pili, Bayern inayofundishwa na kocha Mspanyola, Pep Guardiola ilijikaza na kukataa kuruhusu mabao zaidi, hivyo kukubali kutema taji kwa kichapo cha 5-0. 
Real inayofundishwa na Mtaliano Carlo Ancelotti sasa inasubiri mshindi wa jumla wa Nusu Fainali ya pili kesho Uwanja wa Stamford Bridge kati ya wenyeji Chelsea na Atletico Madrid, baada ya sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza Hispania ili kukutana nayo katika fainali Jumamosi ya Mei 24, mwaka huu Uwanja wa Sport Lisboa mjini Benfica Ureno.
Kikosi cha Bayern Munich kilikuwa: Neuer, Lahm, Dante, Boateng, Alaba, Schweinsteiger, Kroos, Ribery/Gotze dk73, Muller/Pizarro dk73 na Robben, Mandzukic/Martinez dk46.
Real Madrid: Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos/Varane dk75, Coentrao, Alonso, Modric, Di Maria/Casemiro dk84, Ronaldo, Bale na Benzema/Isco dk80.
Real madrid yafuzu kwa fainali ya kombe la mabingwa bara Uropa
Vigogo wa ligi kuu ya Uhispania Real Madrid, wamekuwa timu ya kwanza kufuzu kwa fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya baada ya kuinyeshea Mabingwa watetezi wa kombe hilo Bayern Munich ya Ujerumani kwa mabao manne kwa nunge na hivyo kuibuka a ushindi mkubwa wa jumla ya mabao 5-0.
Sergio Ramos alifunga mabao mawili mapema katika kipindi cha kwanza cha mechi hiyo.
Kabla ya nyota wa Ureno na mchezaji bora duniani Christiano Ronaldo kuihakikishia Madrid fainali yao ya kwanza tangu mwaka wa 2002 na mkwaju wa wa freekick.
Bao hilo lilikuwa lake la 16 katika ligi ya mabingwa barani Uropa.
Kwa Bayern, kichapo hicho kilikuwa ni kama wembe wa kutu kwao kwani mwaka uliopita Wajerumani hao waliifunga Barcelona 7-0 katika hatua ya nusu fainali kabla ya kuilaza Borussia Dortmund na kutwaa taji lao la tano barani ulaya.
Haijulikani kufikia sasa iwapo halmashauri inayoingoza klabu hiyo itachukua hatua yeyote dhidi ya kocha wa klabu hicho Pep Guardiola ambaye licha ya kuiongoza Barca kutwaa taji la Bundesliga ameshindwa kutetea hadhi ya klabu
hiyo katika mchuano huu wenye kitita kikubwa zaidi.
Madrid sasa inasubiri kujua iwapo itachuana na Chelsea ya Uingereza chini ya ukufunzi wake aliyekuwa kocha wao Jose mourinho ama wapinzani wao wa mji wa Madrid , Athletico .
Mshambulizi wa Athletico Madrid Diego Costa alisema anatumai Chelsea hawata regesha basi kwenye lango lao ilhali watacheza mchezo yenye maarifa.
Timu hizo zilitoka sare tasa katika mkondo wa kwanza .

0 comments:

Post a Comment