Dawa hizo hutolewa kwenye vituo maalum vilivyopo ndani ya hospitali
za Mwananyamala, Temeke na Muhimbili, ambako watumiaji hufika kupata
dozi kila siku.
Waandishi wa habari waandamizi wanaofanya mradi wa Fellowship
unaopinga matumizi ya dawa za kulevya chini ya ufadhili wa Mfuko wa
Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), walielezwa hayo wakati wa mafunzo
yanayoendelea kabla ya kuanza kwa mradi huo.
Akizungumza na waandishi hao, Dk. Cassian Nyandidi anayesimamia
utoaji wa Methadone, alisema lengo la ugawaji wa dawa hiyo ni kuokoa
kundi la vijana linaloangamia kutokana na matumizi ya dawa za kulevya.
Kwa mujibu wa mtaalam huyo, kituo cha Mwananyamala kinahudumia waathirika 696, Temeke 119 na Muhimbili 899.
“Watumiaji wa dawa za kulevya ni wenzetu, wanahitaji msaada wetu,
hasa wa matibabu, tukiwaacha tunaongeza ukubwa wa tatizo badala ya
kudhibiti au kumaliza kabisa,” alisema Dk. Nyandidi.
Aliishauri jamii kuondokana na fikra potofu juu ya dawa hiyo huku
akiipongeza serikali kwa kuruhusu tiba hiyo, kwani waathirika wengi wa
dawa za kulevya ni vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa.
0 comments:
Post a Comment