pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Promota wa Diamond mbaroni Ujerumani

 Awin Williams Akpomie 

POLISI nchini Ujerumani wamefanikiwa kumtia mbaroni promota Awin Williams Akpomie, aliyeratibu shoo ya mwanamuziki wa Tanzania, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ iliyokuwa ifanyike Agosti 30, mjini Stuttgart na kushindwa kufanyika.
Shoo hiyo haikufanyika kutoka na mashabiki kuanzisha vurugu kubwa ukumbini wakikerwa na kitendo cha Diamond kukawia kutumbuiza kwa saa tano, vurugu ambazo zilisababisha athari kwa baadhi ya watu kuumizwa na vitu kuharibiwa.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka nchini Ujerumani, Jeshi la Polisi nchini humo watamchukulia hatua za kisheria ili kuwa fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.
Katika tukio hilo, uharibifu mkubwa ulitokea ikiwemo kuvunjwa kwa vyombo vya muziki na vitu mbalimbali na kuna habari kuwa, promota huyo aliuhadaa utawala wa ukumbi huo wa Sindfingen kwamba angefanya African Party na mkutano si onyesho la muziki.
Habari zinasema, vurugu hizo zimesababisha hasara inayofikia Euro 300,000 sawa na sh. Mil.600 za Kitanzania ambazo anatakiwa azilipe.
Aidha, imeelezwa Akpomie hakuwa na bima ya kulinda onyesho hilo na ukumbi ambao ungetumiwa kwa onyesho hilo ambao ni kwa mikutano na maonyesho ya bidhaa si masuala ya muziki.
Taarifa za kipolisi zinasema, suala hilo tayari zimepeleka ofisi ya Sheria ya mji wa Stuttgart zilikotokea fujo hizo kwa hatua zaidi huku polisi wakiendelea kumshikilia kwa mahojiano Akpomie kukiwa na tetezi amekuwa akijihusisha pia na biashara haramu.
Aidha, taasisi mbali mbali na jumuiya za Wafrika nchini Ujerumani na jirani zimelaani vikali tabia za raia huyo kuwadanganya mashabiki na kulivunjia hadhi sifa za bara la Afrika.

0 comments:

Post a Comment