pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Al-Shabaab 'yasambaratika' baada ya mashambulizi ya anga, uasi

Wanajeshi wa Somalia wakiangalia miili ya wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab waliouawa wakati wa mapigano ya kufyatuliana risasi mjini Mogadishu hapo tarehe 26 Disemba, 2014, siku moja baada ya wanamgambo kushambulia makao makuu ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia. AMISOM ilisema kwamba wanajeshi wake walirejesha udhibiti wa kambi hiyo mjini Mogadishu baada ya mapigano ya bunduki kuua washambulizi watano na wengine watatu kukamatwa.  [Na Mohamed Abdiwahab/AFP]Huku viongozi wa al-Shabaab wakiuawa katika mashambulizi ya anga yaliyolengwa na wapiganaji wake kuasi kwa idadi kubwa, serikali ya Somalia na washirika wake wana fursa ya kutumia faida ya hali dhaifu ya kundi hilo, wachambuzi wanasema.
  • Wanajeshi wa Somalia wakiangalia miili ya wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab waliouawa wakati wa mapigano ya kufyatuliana risasi mjini Mogadishu hapo tarehe 26 Disemba, 2014, siku moja baada ya wanamgambo kushambulia makao makuu ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia. AMISOM ilisema kwamba wanajeshi wake walirejesha udhibiti wa kambi hiyo mjini Mogadishu baada ya mapigano ya bunduki kuua washambulizi watano na wengine watatu kukamatwa.

  • "Hasara ambayo al-Shabaab imekuwa ikipata kwa mfululizo katika miaka miwili iliyopita inaonekana kuwa ni tishio kwa uwepo wa kundi hilo," alisema Abdirahim Isse Addow, mkurugenzi wa Redio Mogadishu inayoendeshwa na serikali na msemaji wa zamani wa Umoja wa Mahakama za Kiislamu, umoja ambalo al-Shabaab ilijitenga nalo.
    "Ishara za kutengana kwa al-Shabaab ni dhahiri sana," Addow aliiambia Sabahi. "Hakuna kikundi kinaweza kuendelea kuwepo wakati kinapoteza uungwji mkono na jamii ambayo ipo ndani yake."
    Kutokana na matokeo ya mashambulizi ya Seriklai ya Somalia na Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika Somalia, (AMISOM), al-Shabaab imepoteza mapato ambayo ilikuwa ikipata kutoka miji muhimu kama vile Barawe, Kismayu, Bulo Burde na El Bur, alisema.
    Aidha, alisema, migogoro ya ndani ya al-Shabaab, ambayo imeikumba kikundi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, imekuwa na athari za kudumu katika kuvunja uongozi wa kikundi hicho.
    Migawanyiko ndani ya kikundi hicho ilikuwa mikubwa sana ambayo hatimaye ilipelekea kiongozi wa zamani wa al-Shabaab Ahmed Abdi Godane kuandaa mauaji ya makamanda wengi wa zamani, ikiwa ni pamoja na mwanzilishi mwenza wa al-Shabaab Ibrahim Meeaad al-Afghani, mpiganaji jihadi mzaliwa wa Marekani Abu Mansour al-Amriki na Maalim Burhan, Addow alisema.
    "Baada ya hapo, watu wengine wengi ambao waloikuwa sehemu ya kikundi hicho walikimbia, wakiwemo Mukhtar Robow, Hassan Dahir [Aweys] na Zakariya [Ismail Ahmed Hersi], ambaye hatimaye alijisalimisha kwa serikali," alisema.
    Kikundi hicho kamwe hakikurejea kuotka hali ya kuvunjika katika uongozi wake, ambao sasa umekuwa ukimalizwa kwa mashambulizi ya anga yanayowaua viongozi waliobakia, Addow alisema.
    Katika mfano wa karibuni zaidi wa shambulio la anga lililofanikiwa dhidi ya uongozi wa al-Shabaab, mkuu wa upelelezi wa kikundi hicho Abdinasir Hassan Barakobe, ambaye majina yake mengine yalikuwa ni pamoja na Abdishakur na Tahlil, aliuawa tarehe 29 Disemba karibu na Saakow, kwenye Mkoa wa Jubba ya Kati nchini Somalia.
    Kifo chake kilikuja siku mbili baada ya kujisalimisha kwa mkuu wa upelelezi wa al-Shabaab Hersi kwa mamlaka za Somalia.
    Kabla ya kuuawa, mengi yalikuwa hayajulikani kuhusu Barakobe, ambaye alikuwa katika umri wa miaka 30 na alizaliwa katika familia maarufu huko wilaya ya Bondhere mjini Mogadishu. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Umoja wa Mahakama za Kiislam na baadaye alijiunga al-Shabaab mwaka 2007
    Barakobe alikuwa akiaminika kuwa alikuwa karibu sana na Godane na baada ya kifo chake iliibuka kuwa yeye ndiye aliyekuwa na dhamana wa kitengo cha upelelezi cha Amniyat

    Fursa ya kuiangamiza al-Shabaab

    "Serikali ya Somalia ina fursa kubwa ya kuliangamiza kundi hili kwa msaada wa washirika wake," alisema Abdirisaq Mohamed Qeylow, ambaye alikuwa msemaji wa Muungano wa Mahakama za Kiislamu kabla ya kujiunga na serikali ya Somalia na kuwa msemaji wa Wizara ya Habari chini ya Rais Sheikh Sharif Sheikh Ahmed wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho.
    "Kipindi cha msamaha kinapaswa kuongezwa na fursa zilizotolewa kwa watu ambao hawajafanya makosa makubwa, kama vile vijana, lazima ziongezwe kama vile elimu, kazi na kuwahakikishia usalama wao kama njia ya kuwavutia vijana ambao bado wamo kwenye kundi hilo," aliiambia Sabahi.
    Hatima ya wanachama wa al-Shabaab ni katika ya vigawe vitatu, kwa mujibu wa Qeylow.
    "Kwanza ni viongozi wakuu wa kundi hilo, ambao baadhi yao wamefanya makosa makubwa dhidi ya watu wa Somalia," alisema. "Haitawezekana kwao kujificha ndani ya jamii na serikali ya Somalia haiwezi kufanya maamuzi juu yao peke yake ikiwa watajisalimisha kwa sababu wamefanya makosa makubwa dhidi ya dunia. Hivyo, watajaribu kupigana hadi wauawe."
    "Kuna kundi la pili. Hawa ni watu ambao hawafahamiki sana na watu, lakini wana nguvu kwenye kundi hilo. Hao ni watu walio na fursa ya kujisalimisha na kujitenga mbali na shughuli walizokuwa wakijihusisha nazo wakiwa sehemu ya al-Shabaab," alisema. "Kundi la tatu ni wanachama vijana wa al-Shabaab ambao wanabeba silaha. Hao hujisalimisha kila siku na na kurekebishwa kitabia."
    "Kundi hili halitaweza kuendelea kubakia kama mambo yanakwenda kama hivi," Qeylow aliongeza.
    Ugumu wa al-Shabaab katika kuwabakisha wapiganaji wake wa kigeni na kuwavutia wapya pia unaonesha matatizo ya kundi hilo.
    "Katika siku za karibuni kumekuwa hakuna habari juu ya wapiganaji wa kigeni wanaopigana upande wa al-Shabaab. Nadhani wengi wao wameondoka nchini na wamejiunga na mapigano yanayoendelea kwenye nchi za Kiarabu kama Libya, Yemen na Syria," alisema Qeylow. "Jambo hilo limedhoofisha nguvu za al-Shabaab, ambayo mwanzoni ilikuwa inaungwa mkono kiitikadi na kifedha na al-Qaida."
    "Inawezekana kwamba baada ya kuuawa kwa Fazul Abdullah Mohammed, ambaye alikuwa mkuu wa al-Qaida kwenye eneo la Afrika Mashariki na aliyekufa kwenye mtego wa Godane, na barua ya malalamiko iliyoandikwa na Ibrahim al-Afghani, ambaye pia aliuawa na Godane, kulishusha uungaji mkono wa al-Qaida na makundi mengine (kwa al-Shabaab)," alisema.

    Kupambana na itikadi ya al-Shabaab

    Wimbi la kushindwa lililoikumba al-Shabaab katika siku za karibuni limeufanya uongozi wake kusambaratika na kundi hilo kudhoofika, alisema mchambuzi wa masuala ya kisiasa Hassan Sheikh Ali, lakini itikadi kali ambalo kundi hilo linaisambaza itaendelea nchini Somalia kwa miaka mingi ijayo.
    "Al-Shabaab imekuwa ikienda chini kwa miaka mitatu iliyopita, lakini mauaji ya hivi karibuni ya viongozi wao wa juu yatatumika kwa kuharibu [kudumu] uwezo wa kijeshi wa kundi, nguvu na ari hivi karibuni," Ali aliiambia Sabahi. "Lakini kama itikadi, al-Shabaab itakuwa hapa kwa muda mrefu na itabi8di ipigwe vita kwa itikadi nyingine."
    "Al-Shabaab inaumia pia kwa sababu wapiganaji wa kigeni waliokuwa wakija hapa kwa ajili ya jihadi sasa wanakwenda Syria na Iraq," alisema. "Kwa hivyo, serikali ya shirikisho ya Somalia, serikali za mikoa na majimbo, na jamii ya kimataifa lazima zichukue fursa kwa hali ya kudhoofika ya al-Shabaab iliyonayo sasa."
    "Ili kufanya hivyo, serikali lazima iepuke migogoro ya kisiasa ambayo inaudhoofisha uwezo wake wa kufanya kazi," alisema.
    Kundi kama al-Shabaab linaweza tu kudumu ikiwa lina uongozi imara, alisema Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa Somalia, Mukhtar Haji Kastaro. "Lakini [msingi wa] al-Shabaab umeharibiwa. Katika miezi michache ya hivi karibuni, viongozi wake wengi wakuu wameuawa na serikali isipoteze fursa hii," aliiambia Sabahi.
    "Baadhi ya hatua ambazo serikali na AMISOM wanapaswa kuzichukuwa ni pamoja na kuchukuwa udhibiti wa haraka wa wilaya zilizo chini ya al-Shabaab ili kutowapa fursa ya kujikusanya tena, kujiingiza kwenye mazungumzo na viongozi wa al-Shabaab wenye msimamo wa wastani na kuendelea kuwaandama [kwa kuwauwa] wale wachache wenye siasa kali waliobakia kwenye kundi hilo."
    "Hilo likifanyika, al-Shabaab inaweza kuharibiwa moja kwa moja ndani ya kipindi cha miezi 12 ijayo kwani inapumua upumzi wake wa mwisho," alisema.

    0 comments:

    Post a Comment