pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

50 wawachoma moto Wairaq



Matakfiri wa Daesh wawachoma moto Wairaq 50


Kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh, limewaua kwa kuwachoma moto Wairaq 50 mjini Hīt kaskazini magharibi mwa mji wa al-Ramadi nchini Iraq. Televisheni ya serikali ya al-Iraqiya imethibitisha habari hiyo na kuongeza kwamba kundi hilo limetekeleza jinai hiyo dhidi ya watu hao kufuatia fatwa iliyotolewa na masheikh wa Kisalafi wa Kiwahabi kwa kutegemea maandishi ya vitabu vya Ibn Taymiya. Ni vyema ifahamike kuwa tangu kundi hilo lilipotekeleza mauaji dhidi ya Muadh al-Kasasbeh, rubani wa Jordan aliyeuawa kwa kuchomwa moto na wanachama wa Daesh, kundi hilo la kitakfiri limeendeleza mlolongo wa jinai hizo ambapo karibu kila siku watu kadhaa huuawa kwa njia hiyo. Kwa mujibu wa habari, siku chache zilizopita, wanachama wa Kidaesh, waliwaua watu wengine 45 katika viunga vya mji wa al-Baghdadi, magharibi mwa Iraq. Awali Wizara ya Ulinzi ya Iraq, ilikuwa imetangaza kuwa jeshi la nchi hiyo limewaangamiza wanachama 23 wa kitakfiri hapo jana Jumamosi katika mkoa wa al-Anbar, sanjari na kuangamizwa silaha kadhaa za kundi hilo katika mashambulizi yaliyofanywa kwa kutumia jeshi la nchikavu.

0 comments:

Post a Comment