pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Kenya kuuza nje mafuta ghafi ya petroli mwakani

Kenya kuuza nje mafuta ghafi ya petroli mwakani
Kenya inatazamiwa kuanza kuuza mafuta ghafi ya petroli katika soko la kimataifa mwaka ujao na hivyo kuitangualia nchi jirani ya Uganda ambayo iligundua bidhaa hiyo miaka tisa iliyopita.
Ripoti zinasema kuwa shirika la uchimbaji mafuta na gesi la Uingereza, Tullow linatekeleza mkakati wa kuanza kuzalisha mafuta ya petroli katika eneo la Lokichar kaskazini mwa Kenya.  Awali shirika hilo lilikuwa limesema lingeanza kuuza nje mafuta ya Kenya mwaka 2018 lakini sasa limezidisha kasi ya uchimbaji wa mafuta na hivyo kutoa msukumo mkubwa wa uchumi wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Shirika la Tullow limesema linataraji bomba kutoka Lokichar hadi bandarini eneo la pwani litakuwa tayari ili kuwezesha mafuta ghafi ya Kenya kufika katika soko la kimataifa kabla ya kumalizika mwaka 2016. Inatazamiwa kuwa  Kenya itaanza kwa kuuza mapipa laki moja ya mafuta ghafi ya petroli ya siku. Kwa bei ya sasa ya dola 50 kwa pipa, nchi hiyo inaweza kupata pato la takribani dola bilioni 1.825 au shilingi bilioni 166 kwa mwaka. Kuanza kuzalishwa mafuta ya Petroli mwisho  wa mwaka 2016 kutasadifiana na wakati ambao Wakenya watakuwa wakijirayarisha kwa uchaguzi wa mwaka 2017 na hivyo mafanikio hayo yanatazamiwa kupigiwa debe na serikali ya Jubilee inayoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta.

0 comments:

Post a Comment