pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

EU yaonya juu ya njama za kuigawa Masjidul Aqsa

EU yaonya juu ya njama za kuigawa Masjidul Aqsa
Umoja wa Ulaya umetahadharisha juu ya njama zinazofanywa na utawala haramu wa Israel za kutaka kuugawa msikiti mtakatifu wa al-Aqsa huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu. Ripoti ya EU iliyochapishwa kwenye gazeti la The Guardian la Uingereza inasema kuwa, kuendelea ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi zilizoghusubiwa za Palestina, kushadidi njama za kuigawa Masjidul Aqsa  pamoja na hujuma za kila mara za Wazayuni dhidi ya Wapalestina kunahatarisha mustakabali wa Mashariki ya Kati na kwamba hali hiyo inazidi kuzuia uwezekano wa kuweko kile kinachotajwa kuwa ni ‘suluhu kwa njia ya mataifa mawili’. Ripoti ya umoja wa Ulaya pia imeashiria udharura wa kushinikizwa zaidi utawala haramu wa Israel ili ukubali kurudi kwenye meza ya mazungumzo na Wapalestina bila masharti. Umoja wa Ulaya umesema Israel inapaswa kuheshimu sheria zote za kimataifa na kusimamisha mara moja ujenzi zaidi wa vitongoji kwenye ardhi za Wapalestina.

0 comments:

Post a Comment