pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Iran: Matamshi ya Stephen Harper ni ya kipumbavu

Iran: Matamshi ya Harper ni ya kipumbavu
Msemaji wa Wizara ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali matamshi ya Waziri Mkuu wa Canada, Stephen Harper na kuyataja kuwa ya kijuba na kipumbavu. Bi. Marzie Afkham amesema madai ya Harper kwamba Wairani wanaishi chini ya utawala wa kiimla yanaonyesha jinsi kiongozi huyo alivyo na chuki dhidi ya taifa hili. Kwenye hotuba yake ya siku ya Jumamosi mbele ya Wairani wanaoishi Canada, Waziri Mkuu Stephen Harper alidai kwamba Iran inaendeshwa kidikteta na kwamba raia wa nchi hii hawajui ladha ya demokrasia. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Harper anajaribu kutumia madai ya uongo ili kuwashawishi Wairani wenye uraia wa Canada waunge mkono chama chake kwenye uchaguzi ujao wa bunge.
Uhusiano wa Iran na Canada ulivurugika zaidi mwaka 2012 baada ya serikali ya Ottawa kutangaza kuwa imefunga ubalozi wake hapa mjini Tehran na baadaye kuanza kutoa madai ya uongo na ya kipropaganda dhidi ya viongozi na serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

0 comments:

Post a Comment