pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Marais wa nchi 6 za Afrika kukutana TZ Leo

Marais wa nchi 6 za Afrika kukutana TZ kesho
Marais wa nchi sita za Afrika watakuwa na mkutano mkubwa jijini Dar es Salaam, Tanzania hapo kesho ambapo watajadili kwa kina juu ya kuboresha uwekezaji katika kanda ya Maziwa Makuu. Marais hao ni Joseph Kabila wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Pierre Nkurunziza wa Burundi, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenyeji wao wa Tanzania, Rais Jakaya Kikwete. Mkutano huo wa siku mbili utaambatana na mdahalo baina ya viongozi hao na wadau mbalimbali katika sekta za biashara na maendeleo. Mjadala wa viongozi hao utajikita katika umuhimu wa Ukanda wa Kati ambao ni kiungo muhimu katika ukuaji uchumi wa nchi hizo kwa kuwa husaidia katika uingizaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali kupitia Tanzania kwa njia za maji, reli na barabara. Wakati wa mkutano huo, viongozi hao watafanya uzinduzi wa treni ya mizigo kuelekea Uganda, Rwanda na DRC.

0 comments:

Post a Comment