pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Iran na kundi la 5+1 zafikia makubaliano ya kihistoria

Iran na kundi la 5+1 zafikia makubaliano ya kihistoria
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na madola sita makubwa duniani yanayounda kundi la 5+1 yamefikia makubaliano muhimu na ya kihistoria kuhusiana na miradi ya nyuklia ya Iran. Kwa mujibu wa makubaliano hayo Iran itaondolewa vikwazo vyote ilivyokuwa imewekewa. Matini ya makubaliano hayo inasema kuwa, vikwazo vyote vya kifedha, kiuchumi, kibenki, mafuta, gesi, petrokemikali, kibiashara, bima na usafiri na uchukuzi ilivyokuwa imewekewa Iran vitaondolewa baada ya jambo hilo kupasishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Aidha marufuku iliyokuwa imewekewa Iran ya kununua ndege za abiria nayo imeondolewa. Taarifa zaidi kuhusiana na makubaliano hayo itakujieni katika matangazo yetu ya leo usiku.

0 comments:

Post a Comment