pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

'Saudia yatumia silaha zilizopigwa marufuku Yemen'

'Saudia yatumia silaha zilizopigwa marufuku Yemen'
Mjumbe wa harakati ya wananchi ya Answarullah nchini Yemen, ameituhumu Saudia kwa kutumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa dhidi ya raia wa nchi hiyo. Ahmad Hashim aliyasema hayo jana Jumapili alipokuwa akizungumza na Shirika la Habari la Fars News na kuongeza kuwa, licha ya Umoja wa Mataifa kutangaza kusimamishwa vita nchini Yemen, lakini Saudia na waitifaki wake wameendelea kuwashambulia raia wa Yemen kwa silaha zilizopigwa marufuku kimataifa. Hashim ameongeza kuwa, baadhi ya nchi za Magharibi hususan Marekani zinaunga mkono mashambulio hayo ya Saudia nchini Yemen na zinashirikiana na utawala huo wa kifalme wa ukoo wa Aal Saud katika kutenda jinai hizo. Kiongozi huyo wa harakati ya Kiislamu ya Answarullah, amesisitiza kuwa, utawala wa Aal Saud unafanya jinai hizo kwa makusudi mbele ya kimya cha jamii ya kimataifa huku ukikanyaga waziwazi sheria za kimataifa. Ijumaa iliyopita, Umoja wa Mataifa ulitangaza kusitishwa vita kuanzia siku hiyo hadi mwishoni mwa mwezi wa Ramadhani kwa lengo la kufikisha misaada ya dharura kwa wahanga wa mashambulizi hayo nchini Yemen, hata hiyo Saudia ilikengeuka usitishaji vita huo, saa chache baada ya kutangazwa ikidai kuwa haikujua kuwa kuna usitishaji huo wa vita na wala haikuombwa kufanya hivyo na kibaraka wake, Mansour Hadi.

0 comments:

Post a Comment