pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

DAESH WAUA KUNDI LA WATU KTK MJI WA NICE, UFARANSA

Zaidi ya watu 84 wameripotiwa kuuawa katika shambulio lililotokea katika mji wa Nice kaskazini mwa Ufaransa.
Lori lililokuwa likienda mwendo wa kasi lilijipenyeza katika mkusanyiko wa watu waliokuwa wakishiriki maonesho ya fataki kuadhimisha siku ya kitaifa ya Bastille, ambayo huandamana na shamra shamra kila mwaka. Polisi walifanikiwa kumuua dereva wa lori hilo baada ya kujiri majibizano ya risasi yaliyochukua muda mrefu kwenye tukio hilo. Kamanda wa polisi wa mji wa Nice amekielezea kitendo cha dereva huyo kuwa cha kigaidi na amewataka wananchi kuchukua tahadhari. Kundi la Daesh limekiri kuhusika na shambulio hilo lililotokea nchini humo wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Bastille. Rais François Hollande wa Ufaransa, sanjari na kulaani shambulizi hilo, amedai kuwa, nchi yake itaendeleza mashambulizi dhidi ya wanachama wa kundi hilo, nchini Syria. Inafaa kuashiria hapa kwamba, Ufaransa ni moja ya nchi waungaji mkono kwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh nchini Syria kwa lengo la kutaka kuiondoa madarakani serikali halali ya Rais Bashar al-Assad wa nchi hiyo

0 comments:

Post a Comment