pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

BUNGE LA MAREKANI LAIWEKEA VIKWAZO IRAN


Sambamba na kutimia mwaka mmoja tangu kufikiwa makubaliano ya nyuklia kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kundi la 5+1, baraza la wawakilishi nchini Marekani, limepasisha vikwazo vipya dhidi ya taifa hili.
Jana baraza la wawakilishi nchini Marekani ambalo linaundwa na silimia kubwa ya wawakilishi kutoka mrengo wa chama cha Republican, lilipitisha mpango wa vingee viwili wa vikwazo hivyo kwa kupigiwa kura ya ndio na wajumbe 246 kati ya 179 waliopinga mpango huo. Wawakilishi wa Marekani pia walipitisha kwa kura 246 kati ya 181 mpango wa kupiga marufuku Iran kunufaika na mfumo wa kifedha wa Marekani na pia sarafu ya dola katika miamala yake ya kigeni. Kabla ya hapo pia yaani siku ya Jumatano, baraza hilo la wawakilishi la Marekani lilipiga marufuku ununuzi wa maji mazito kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Miswada hiyo dhidi ya Iran ya Kiislamu imepitishwa katika hali ambayo Rais Barack Obama wa Marekani ametishia kuipigia kura ya veto kuipinga.

0 comments:

Post a Comment