pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Mkulima (54) adaiwa kunajisi mtoto (6)


MKAZI wa wilayani Igunga mkoani Tabora ,Shimba Kanyala (54) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Wilaya hiyo akidaiwa kunajisi.
Mwananchi huyo anakabiliwa na mashitaka ya kumnajisi mtoto mwenye umri wa miaka sita. Kanyala (54) ni mkulima wa kijiji cha Nkinga, tarafa ya Simbo.
Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi, Wilaya ya Igunga, Frank Matiku ameieleza mahakama kuwa, Agosti 23, mwaka huu saa 10 jioni katika kijiji cha Nkinga, mshitakiwa alimnajisi mtoto na kumsababishia maumivu sehemu zake za siri.

0 comments:

Post a Comment