Umekua ni usafiri mwingine mzuri na wenye starehe yake kama ukipata
nafasi ya kuutumia kwenye nchi zilizoendelea kama Marekani, Uingereza
Dubai na kwengineko ambako kuna watu wengine wanategemea sana kuutumia
na kuacha magari yao nyumbani na kujikuta wamewahi town na kumaliza
shughuli zao manake hamna foleni.
Dar es salaam likiwa jiji la tisa kwa ukuaji duniani huku kwa Afrika
likishika nafasi ya tatu, limekua na foleni kubwa ambazo mamlaka ya
mapato Tanzania (TRA) inasema huwa kila siku inapatikana hasara ya
shilingi BILIONI TATU kutokana na foleni Dar es salaam.
Elisha Elia alimuuliza Mwakyembe… Je umeme wa bongo tunavyoufahamu na
historia yake utafaa kuuwezesha usafiri huo wa Treni kufanya kazi yake?
manake treni hizi za kasi zinatumia umeme.
Akajibiwa ‘hawatotumia umeme wa TANESCO, watatumia umeme wa solar na
vyanzo vingine vya umeme ili isitokee treni ikasimama katikati manake
umeme ni lazima uwepo kwa saa 24′
CRD: MILLARDAYO .COM






0 comments:
Post a Comment