pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Ajifungua salama bwenini, walimu wamsaidia

Dodoma. Mwanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Sekondari Mbabala, Manispaa ya Dodoma, Helena Mpondo amejifungua mtoto ndani ya bweni.
Mwanafunzi huyo amejifungua mtoto mwenye afya njema kwa usaidizi wa walimu na baadaye aliitwa mganga wa zahanati ya jirani kwa ajili ya kumkata kitovu na msaada mwingine.
Helena, Ijumaa ya Septemba 2 saa tatu asubuhi alizidiwa na uchungu akiwa peke yake bwenini, lakini matroni na mwalimu mwingine wa kike waliwahi kufika eneo hilo na kumsaidia kujifungua salama.
Mkuu wa shule hiyo, Joram Mkwawa amesema siku ya tukio, saa tatu asubuhi aliitwa na walimu wenzake bwenini na alikuta binti huyo amejifungua.
“Nilichofanya niliwaambia waende zahanati na nilituma pikipiki ya kumfuata mzazi wake ambaye alipofika, nilimkabidhi mwanawe kwa kuwa ni kosa kukaa na mtoto mwenye mimba,” amesema.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Christina Mndeme alitoa taarifa kuwa manispaa hiyo ilikuwa na wanafunzi 51 wenye mimba na kati yao, 45 walikuwa wa shule za sekondari na sita wa shule za msingi.

0 comments:

Post a Comment