pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Akatwa Ulimi Kwa Meno Akila Denda

Katika hali isiyokuwa ya kawaida kijana aliyejulikana kwa jina Said Juma amelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Singida baada ya kung’atwa hadi kunyofolewa zaidi ya theluthi moja ya ulimi wake na mwanamke anayetuhumiwa kufanya naye mapenzi hali iliyomfanya apoteze uwezo wa kuongea zaidi ya kutoa maelezo kwa njia ya maandishi.
Akizungumza kwa njia ya maandishi kijana huyo aliyelazwa katika chumba cha wagonjwa wa kinywa na meno amesema kuwa siku ya tukio akiwa njiani kutoka kwenye
sherehe za Idd El Hajj alikutana na mwanamke jirani akinywa pombe katika glocery moja ambaye alimuomba amsindikize nyumbani kwake.
Kijana huyo anaeleza kuwa akiwa njiani,mwanamke huyo alimtaka kijana huyo wafanye mapenzi na baada ya kumkatalia alimuomba amuage kwa kumpa ulimi “kula denda” ndipo alipomng’ata hadi kumnyofoa kipande cha ulimi na kutoweka nacho.
Madaktari wanaomtibu kijana huyo wanasema kidonda hicho baada ya kuacha kutoa damu kilitengeneza maambukizi kukawa na harufu inatoka mdomoni na kwamba hali yake inaendelea vizuri.
Wamesema ingawa amepata ulemavu lakini kijana huyo anaweza kuongea tena baada ya kupona japo matamshi yake ya maneno hayatakuwa kama alivyokuwa anaongea mwanzo.
Mama mzazi wa kijana huyo tayari ameripoti tukio hilo kituo cha polisi kwani mbali na mtoto wake kupata ulemavu pia alipata kipigo kutoka kwa mwanamke huyo.
Bado mtuhumiwa hajakamatwa na polisi wanafanya ufuatiliaji.
Chanzo- Kipindi cha Matukio Radio Free Africa

0 comments:

Post a Comment