pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

New Force Dar - Songea Laua na Kujeruhi


Basi la New Force kutoka Dar es salaam kwenda Songea
limepata ajali baada ya kupinduka eneo la Kifanya kilomita kadhaa kutoka mkoani Njombe.
Ajali hiyo imetokea Septemba 19,2016 majira ya saa moja na dakika 40 usiku.
Inaelezwa kuwa watu 12 (wanawake 8,wanaume 4) wamepoteza maisha huku 9 wakijeruhiwa.
Abiria wa basi hilo wanasema basi lilikuwa katika mwendo kasi na kwamba lilinusurika kupinduka mara mbili na mara ya tatu ndipo likapinduka.
Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe ACP Prudenciana Protas amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

0 comments:

Post a Comment