pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

RAIS JAKAYA KIKWETE NA MKEWE MAMA SALMA WATEMBELEA MTAA WA INDRA GHANDI NA KUWAPA POLE WAATHIRIKA

MHE Kikwete aliwasili mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam leo akiwa ameongozana na mkewe Mama Salma Kikwete kujionea mwenyewe jengo lililoporomoka asubuhi saa mbili na nusu leo Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zinaendelea kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia.jengo lililoporomoka lilikuwa la  ghorofa la 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri.POLENI SANA TANZANIA. TUSHIKAMANE KUWAFARIJI WOTE WALIOATHIRIKA NA JANGA HILI
MHE Kikwete aliwasili mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam leo akiwa ameongozana na mkewe Mama Salma Kikwete kujionea mwenyewe jengo lililoporomoka asubuhi saa mbili na nusu leo Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zinaendelea kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia.jengo lililoporomoka lilikuwa la ghorofa la 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri.POLENI SANA TANZANIA. TUSHIKAMANE KUWAFARIJI WOTE WALIOATHIRIKA NA JANGA HILI
hapa DAR ES SALAAM LEO ni msiba na majonzi ni baada ya kuporomoka kwa  jengo la ghorofa kumi na tano linalomilikiwa kwa ubia kati ya Shirika la Nyumba la Taifa NHC na kampuni ya Aliraza Investiments Ltd ya jijini Dar es salaam huku mjenzi wa jengo hilo ikiwa ni kampuni ya ujenzi ya Luck Construction Ltd, mpaka sasa uokoaji unaendelea lakini ukionekana kusuasua kutokana na ufinyu wa eneo lenyewe na vifaa hafifu vya kuokolea, bado haijafahamika kwamba ni watu wangapi wamepoteza maisha katika ajali hiyo na wangapi wamejeruhiwa , magari ya kubebea wagonjwa yamekuwa yakipishana mara kwa mara wakati yakipeleka ama majeruhi ama watu waliopoteza maisha katika tukio hilo la kusikitisha.
 Ni msiba na majonzi ni baada ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa kumi na tano linalomilikiwa kwa ubia kati ya Shirika la Nyumba la Taifa NHC na kampuni ya Aliraza Investiments Ltd ya jijini Dar es salaam huku mjenzi wa jengo hilo ikiwa ni kampuni ya ujenzi ya Luck Construction Ltd, mpaka sasa uokoaji unaendelea lakini ukionekana kusuasua kutokana na ufinyu wa eneo lenyewe na vifaa hafifu vya kuokolea, bado haijafahamika kwamba ni watu wangapi wamepoteza maisha katika ajali hiyo na wangapi wamejeruhiwa , magari ya kubebea wagonjwa yamekuwa yakipishana mara kwa mara wakati yakipeleka ama majeruhi ama watu waliopoteza maisha katika tukio hilo la kusikitisha.

1 comments:

  1. tanzania na matukjo ya ajabu mpaka lini jamani!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete