pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Polisi Rukwa wadaiwa kuua mtuhumiwa wa wizi

 
Sumbawanga. Mtuhumiwa wa wizi, Christopher Sanga ‘Chinga’ (30), amefariki dunia katika chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga baada ya kufyatuliwa risasi na polisi.
Taarifa kutoka hospitalini zinasema mtuhumiwa huyo alijeruhiwa na risasi iliyompiga kwenye nyonga kisha kutokea katikati ya makalio na alifariki dunia juzi wakati madaktari wakijitahidi kuokoa maisha yake.
Pia askari wa Kikosi cha Upelelezi wilayani Sumbawanga, Rock Mnubi (31) naye anaendelea kutibiwa katika hospitali hiyo alikolazwa baada ya kujeruhiwa kwa fyekeo kichwani na mtuhumiwa.
Kwa mujibu wa mke wa marehemu, Halima Mlongo (27), askari polisi watano walifika nyumbani kwake wakiwa wamevaa kiraia, huku wawili kati yao wakiwa na bunduki kila mmoja.
Alidai kuwa walipofika nyumbani hapo waliianza kuikagua nyumba hiyo, huku yeye akiwa dukani baadaye walimwamuru amtafute mume wake, yeye aliingia chumbani na kumweleza mumewe kuwa ana wageni wanamsubiri nje.
Aliongeza kuwa “Askari hao walipiga teke mara mbili na mlango ukafunguka kisha marehemu akajihami kwa kumkata na fyekeo mmoja wa askari hao na mwingine kuoana mwenzake amejeruhiwa, alimfyatulia mume wangu risasi moja na akaanguka chini huku akivuja damu nyingi.”
Jirani wa marehemu, James Nkondya ambaye alishuhudia tukio hilo alisema kuwa askari hao hawakumwarifu hata mwenyekiti wao wa kitongoji ambaye alifika hapo baada ya askari hao kumpiga risasi Chinga kisha kuondoka zao.
Ndugu wa marehemu huyo walifika mjini hapa kutoka Makete, walikataa kuuchukua mwili wa marehemu na kuandamana hadi Kituo cha Polisi wakitaka kuelezwa sababu ya kifo, huku wakitishia kuwa iwapo polisi wakiamua kumzika wenyewe watakiona.
Baba mdogo wa marehemu, Damian Mbilinyi alisema walipofika Kituo Kikuu cha Polisi mjini hapa waliambiwa waonane na Ofisa Upeleleizi wa Mkoa, Peter Ngusa na kushindwa kuafikiana katika mazungumzo yao, lakini baada ya kubanana nao  polisi walitoa ubani wa Sh1,000,000 na lita 200 za dizeli kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda Makete kwa maziko.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda a mtuhumiwa alipigwa risasi wakati akipambana na polisi waliotaka kumkamata kwa wizi.
Mwaruanda alisema askari huyo na wenzake walifika nyumbani kwa mtuhumiwa huyo mali za Sh2.5 milioni, za Kampuni ya Sumry Enterprises ya mjini Sumbawanga anaodaiwa kutenda Machi 27.

0 comments:

Post a Comment