pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

AJALI: GARI LA KATIBU MKUU WA FEDHA LASHAMBULIWA

VIJANA wasiojulikana wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa kundi la ubaya ubaya, wamelishambulia kwa mawe na mapanga gari la Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar.
Hata hivyo, wakati tukio hilo likitokea Katibu Mkuu Wizara hiyo, Khamis Mussa, hakuwemo.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 3:00 asubuhi katika maeneo ya Mwanakwerekwe nyumba mbili ambapo kwa makusudi vijana hao wanaokisiwa kuwa zaidi ya 40 waliizingira barabara hiyo na kuanza kurusha mawe na kuliharibu gari hilo.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walisema uwa sababu ya vijana kufanya hivyo ni kutokana na wafanyakazi wa Baraza la manispaa,kuwazuia vijana hap wasichimbe mchanga na  kukamatwa ng’ombe wao ambae walikuwa wakimtumia kwa kazi hiyo.
Alisema baada ya ng’ombe wao kuchukuliwa waliamua kukaa barabarani na kuanza kuzishambulia kwa mawe baadhi ya gari za serikali na kuliharibu hari hilo.
Aidha walisema kuwa vijana hao wanaojulikana kwa jina la ubaya ubaya wamekuwa wakikatazwa mara kwa mara kuchimba mchanga lakini hawasikii.
Akizungumza na gazeti hili baada ya tukio hilo dereva wa gari hilo, Haji Mrisho Ali, alisema gari hilo lilishambuliwa wakati akienda nyumbani kwa Katibu Mkuu huyo Chukwani, kumchukua mke wa bosi wake.
Aidha alisema wakati akijihami kwa kukwepa mawe hao, gari hilo lilijigonga na ukuta na kupinduka, hata hivyo hakuna majeraha aliyopata.
Nae  Mkurugenzi Uendeshaji na Utumishi wizara hiyo, Ramadhani Senga Salmini, alisema, vijana hao wana lengo la kuitia hasara serikali kwa hivyo lazima washughulikiwe.
Gari hilo limeharibiwa kwa kuvunja vioo vyote na sehemu nyengine kadhaa.

0 comments:

Post a Comment