pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Atakayekamata CD ‘feki’ kuzawadiwa

KAMPUNI ya Hamadombe Distributor inayomiliki kundi la sanaa la Hamadombe, imetangaza kutoa dau nono kwa yeyote atakayemkamata mtengenezaji ama muuzaji wa CD bandia za filamu ya ‘Yote ni Baba’ iliyo sokoni kwa sasa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, muigizaji wa kundi hilo Mary Joseph ‘Vanessao’, alisema kuwa kampuni yao imeamua kutangaza hivyo ili kudhibiti wimbi la hujuma za kazi zao, ambazo wamekuwa wakitumia gharama kubwa kuziandaa, lakini wanaonufaika ni watu wengine.
“Hamadombe inasimamia kazi zake na imetangaza dau hilo, kwa sababu haioni kazi inayofanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Chama cha Haki Miliki Tanzania (Cosota), ambapo licha ya filamu nyingi kuwa na stika ya TRA, lakini bado zinatengenezwa feki na kuingizwa sokoni,” alisema Vanessa.
Alisema kuwa wasanii wote wa kundi hilo huwa wanasambaza wenyewe filamu zinazotengenezwa na Hamadombe Distributor na hutumia pia mwanya huo kuwasaka watu ambao wanafanya mchezo huo mchafu.
Msanii huyo aliwataka pia wasanii wa makundi mengine kupendana ili kudhibiti wimbi hili, kwani serikali imeshindwa kuwasaidia, hivyo ni vema wao wakawa kitu kimoja kusaka kazi feki na kuziondoa sokoni na kwa kufanya hivyo watafanikiwa.
freemedia

0 comments:

Post a Comment