Na
Hafsa Golo
MELI
mpya ya serikali inayotengenezwa nchini Korea Kusini inatarajiwa kuwasili
nchini Febuari 15 mwakani.
Meli
hiyo inayotengenezwa na kampuni ya Posco Plantec, ipo katika hatua nzuri ya
ujenzi wake na itakuwa na uwezo wa kuchukua abiria 1200 na mizigo tani 120.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Meli Kepteini, Alhaj Masoud Sururu, alisema wakati
akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Malindi.
Alisema
kupatikana kwa meli hiyo kutaondosha usumbufu kwa wasafiri wa Pemba
na Unguja.
Alisema
meli hiyo ina uwezo wa kupambana na mawimbi makali wakati wa safari hasa katika
mkondo wa Nungwi na itakuwa inachukua muda wa saa nne kutoka Unguja hadi Pemba
na masaa matatu kwa Unguja hadi Dar esSalamu.
Aliwahakikishia
wananchi kwamba nauli ya meli hiyo itakuwa nafuu tofauti na boti nyengine
zinazomilikiwa na watu binafsi.
Akielezea
kuhusu meli ya Mv Maendeleo alisema kutokana na uchakavu unaoikabili meli hiyo haitochukua
tena abiria na badala yake itakuwa meli ya mizigo na itafanya safari zake kati
ya Unguja, Pemba, Tanga na Dar es Salamu.
Akizungumzia
kuhusu wafanyakazi wa meli hiyo mpya alisisitiza kuwa kwa hivi sasa shirika
lina wafanyakazi wa kutosha hata hivyo kama litaamua kuajiri wafanyakazi wapya kipaumbele
kitatolewa kwa makapteni na mainjinia.
0 comments:
Post a Comment