pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

OFISI YA RAIS, TUME YA MIPANGO YAKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA CHUMA LIGANGA MKOANI NJOMBE


Displaying DSC05807.JPG
Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Dkt. Philip I. Mpango (wa tatu kushoto) akipata maelezo kuhusu Mradi wa Chuma Liganga kutoka kwa Nie Zhiyan (kulia), ambae ni Makamu Afisa Muendeshaji Mkuu wa Tanzania China International Mineral Resources Ltd (TCIMRL). Hili  ni eneo ambalo kiwanda cha chuma chenye uwezo wa kuzalisha tani milioni moja kwa mwaka kitajengwa. Kutoka kushoto, wengine ni Bw. Ramson Mwilangali, Kaimu Mkurugenzi wa Viwanda Mama - NDC , Bw. Erasmus Masumbuko, Mchumi - Tume ya Mipango, Bw. Maduka Kessy, Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango, anaeshughulikia Sekta za Uzalishaji, Bw. Israel Mkojera Makamu Meneja Utawala - TCIMRL, Bi. Florence Mwanry Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango anaeshughulika na Huduma za Jamii na Idadi ya Watu na Bw. Mlingi E. Mkucha, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NDC.

Displaying DSC05819.JPG
Kilima  chenye madini Ya chuma, ambapo  shughuli ya uchimbaji wa chuma unategemea kuanza kutekelezwa. Uzalishaji wa chuma unatarajiwa kuanza mwaka 2016.
Displaying DSC05866.JPG
Viongozi na Maofisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa katika eneo ambalo uchimbaji wa chuma utatekelezwa. Pamoja nao ni Viongozi kutoka National Development Corporation (NDC) na Tanzania China International Mineral Resources Ltd. Nyuma ni kilima ambacho kimejaa utajiri wa mawe yenye madini ya chuma ambapo jiwe linakadiriwa kuwa na chuma kwa 52%.
Displaying DSC05897.JPG
Viongozi na maofisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango (ORTM), National Development Corporation (NDC) na Tanzania China International Mineral Resources Ltd (TCIMR) wakiwa pamoja na viongozi wa kijiji cha Mundindi ambapo ni eneo ambalo Mradi wa Uchimbaji wa Chuma utatekelezwa. Viongozi hawa pamoja na wanakijiji wameonyesha ushirikiano mzuri na mwekezaji katika kufanikisha utekelezaji wa mradi.


Displaying DSC05904.JPG
Timu kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakipata maelezo kutoka kwa wataalam wa kampuni ya Tanzania China International Mineral Resources Ltd kuhusu Iron Ore Samples zilizopatikana wakati wa utafiti kuhusu wingi na ubora wa chuma kitakachopatikana katika eneo la Liganga.

Displaying DSC05918.JPG
Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Dkt. Philip I. Mpango (aliyesimama) akiongea na Viongozi wa Kijiji cha Mundindi pamoja na viongozi na wataalam wa kampuni ya Tanzania China International Mineral Resorces Ltd.

Picha na: Thomas Nyindo.

0 comments:

Post a Comment