pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Hamas na Israel zaafiki usitishaji vita wa masaa 72

Hamas na Israel zaafiki usitishaji vita wa masaa 72
Umoja wa Mataifa na Marekani zimetangaza kuwa, Harakati ya Kiislamu ya Palestina Hamas na utawala pandikizi wa Kizayuni wa Israel, zimekubali kusitisha mapigano kwa muda wa masaa 72, kuanzia asubuhi ya leo Ijumaa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry amenukuliwa akisema kuwa, kuanzia leo asubuhi kwa nyakati za eneo la Ghaza, kutaanza kusitishwa vita na kisha Wazayuni na Wapalestina watakwenda mjini Cairo, Misri kwa minajili ya kuanza mazungumzo. Hata hivyo akizungumza kwa pamoja na Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kerry amesema kuwa katika kipindi hicho cha usitishaji vita askari wa Kizayuni walioko katika maeneo ya vita wataendelea kubakia katika maeneo hayo. Aidha ripoti hiyo imesisitiza kuwa, ni lazima kuchungwa kikamilifu haki za raia katika kipindi hicho. Kwa mara kadhaa pande mbili zimekuwa zikiweka makubaliano ya usitishaji vita, hata hivyo utawala wa Kizayuni umekuwa ukivunja makubaliano hayo kwa kutumia kwa visingizio tofauti na kuanza kushambulia kikatili maeneo ya raia katika Ukanda wa Ghaza.

0 comments:

Post a Comment