pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Wapalestina 150 wauawa kinyama masaa 24 yaliyopita

Wapalestina 150 wauawa kinyama masaa 24 yaliyopita
Utawala katili wa Israel umefanya mauaji ya umati katika mji wa Rafah ulioko kusini mwa Ukanda wa Gaza huko Palestina. Taarifa kutoka Gaza zinasema kuwa, Wapalestina 150 wameuawa shahidi kufuatia mashambulio ya Israel katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita. Mauaji ya jana na leo ya jeshi la Israel huko Gaza yametajwa kuwa ni mauaji ya umati. Weledi wa mambo wamezitaja jinai za utawala wa Kizayuni huko Gaza kuwa ni sawa na jinai zilizotendwa na Adolph Hitler wa Ujerumani enzi za uhai wake. Miongoni mwa waliouawa shahidi katika mashambulio ya kinyama ya Isreal wamo wanawake na watoto wadogo. Wakati huo huo, msemaji wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina la Umoja wa Mataifa UNRWA amesema kuwa hali ya kibinadamu Gaza ni mbaya mno. Wakati ulimwengu mzima ukionesha kusikitishwa na mauaji ya kinyama yanayofanywa na jeshi la Israel dhidi ya Wapalestina, maulama wa Saudia wameendelea kutoa fatuwa za kuwakandamiza Wapalestina. Abdul Aziz Al Sheikh, Mufti wa Saudi Arabia na Mkuu wa Kamati ya Maulama wa nchi hiyo amesema kuwa, kufanya maaandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina wa Gaza ni hatua ya kuleta vurugu na isiyo na faida.  Kwa upande wake Swaleh al-Haidan, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Mahakama la Saudia  ametoa fatuwa ya kuharamisha maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina. Al-Haidan ameongeza kuwa, kufanya maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina ni sawa na kufanya uharibifu katika ardhi.

0 comments:

Post a Comment