pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Marekani yapiga marufuku adhana chuo kikuu Duke

Marekani yapiga marufuku adhana chuo kikuu Duke
Katika mwendelezo wa chuki dhidi ya dini na matukufu ya Kiislamu, Marekani imepiga marufuku adhana katika Chuo Kikuu cha Duke nchini humo. Chuo Kikuu cha Duke ambacho hivi karibuni kilikuwa kimetoa ruhusa kwa Waislamu wa chuo hicho kuadhini, kimepiga tena marufuku suala hilo. Wiki iliyopita, viongozi wa chuo hicho  kilichopo katika jimbo la Carolina kaskazini walitoa taarifa rasmi iliyoruhusu adhana kupitia mnara wa kanisa shuleni hapo. Awali Michael Schoenfeld, Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Duke alinukuliwa akisema kuwa, wanafunzi wa Kiislamu wamekuwa na mchango mkubwa katika ustawi wa chuo na kwamba bodi ya shule inakubali watekeleze ibada zao shuleni hapo. Hata hivyo ghafla viongozi wa chuo hicho wamepiga marufuku adhana bila kutolewa sababu maalumu. Baadhi wanamtaja Franklin Graham, kasisi wa Kimarekani kuwa chanzo cha marufuku hiyo, hasa kwa kuzingatia kuwa hivi karibuni alitishia kukata misaada yake kwa chuo hicho  ikiwa Waislamu wataruhusiwa kuadhini chuoni hapo.

0 comments:

Post a Comment