pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

“Iran haitalegeza kamba katika haki zake za nyuklia” - Rouhan

“Iran haitalegeza kamba katika haki zake za nyuklia”
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran yaani bunge Ali Larijani amesema kuwa serikali ya Iran na wananchi kamwe hawatalegeza kamba juu ya haki zao za kinyuklia. Larijani ameyasema hayo huku Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ikiendeleza mazungumzo yake na kundi la 5+1 ili kufikia makubaliano kamili kuhusu miradi yake ya nyuklia. Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa madola yenye nguvu yanataka kuzuia maendeleo ya Iran katika sayansi ya nyuklia kwa kuibua changamoto katika uga wa kimataifa. Hata hivyo Iran haitaachia haki zake za nyuklia. Larijani amesisitiza kwamba mashinikizo na vikwazo vya madola yenye nguvu havitakuwa na taathira kwa miradi ya nyuklia ya nchi hii yenye malengo ya amani

0 comments:

Post a Comment