pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

HII NDO STORI KUHUSU WALIOKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA KWENYE MELI ILIYO NA USAJILI WA TAZANIA


Meli iliyomatwa huko Glosgow
Watu wawili raia wa Uturuki walionaswa mwaka jana kwenye ufukwe wa Aberdeen, Scotland na meli iliyokuwa imebeba tani tatu za dawa za kulevya aina ya cocaine huku ikiwa na usajili wa nchini Tanzania, wamekutwa na hatia mahakamani nchini Scotland.
Mahakama Kuu ya Glasgow, mji mkuu wa Scotland imewakuta na hatia watu hao ambao ni Mumin Sahin na Emin Ozmen kwa kukutwa na dawa hizo za kulevya daraja A zenye thamani ya Paundi milioni 500 za Uingereza ambazo ni sawa na Shilingi trilioni 1.49 za Tanzania. Aidha mahakama hiyo haikuwakuta na hatia washtakiwa wengine kwenye kesi hiyo ambao ni, Kayacan Dalgakiran, Mustafa Guven, Umit Colakel na Ibrahim Dag. Kwa mujibu wa habari hiyo, dawa hizo za kulevya tani 3.2 aina ya cocaine na zilifichwa ndani ya meli ya MV Hamal iliyokuwa inapeperusha bendera ya Tanzania. Inaarifiwa kuwa, kabla ya hapo meli hiyo, inayomilikiwa na kampuni ya Kiev Shipping and Trading Corporation, ilitia nanga kwa muda nchini Guyana, Amerika ya Kusini ambayo hutumiwa kupakia cocaine kuelekea Amerika Kaskazini na Ulaya. Taarifa zaidi zinasema kuwa meli hiyo iliyokamatwa Aprili 23, mwaka jana, ilikuwa imetia nanga maili 100 kutoka ufukwe wa Aberdeen, Uingereza baada ya kuzuiwa kuingia nchini humo. Hiyo ni meli ya tatu kukakamatwa ikiwa imebeba mzigo mkubwa wa dawa za kulevya baada ya ile iliyokamatwa nchini Italia ikiwa na usajili wa Tanzania ikiwa na tani 30 za cocaine na nyingine ya Canada iliyokamatwa katika Bahari ya Hindi nchini Tanzania ikiwa na kilo 283 za cocaine.

0 comments:

Post a Comment