
NDEGE mpya ya kwanza iliyonunuliwa na serikali kwa ajili ya kutumiwa na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), imetua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam (JNIA), ikitokea nchini Canada ilikotengenezwa.
Ndege hiyo ilitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere majira ya saa 6:15 mchana jana. Baada ya kutua ndege hiyo, ilipatiwa heshima maalumu ambayo hutolewa kwa ndege yoyote mpya inayotua katika...