pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Rais Kikwete ashinda tuzo ya 'Nembo ya Demokrasia'

Rais Kikwete ashinda tuzo ya 'Nembo ya Demokrasia'
Jarida la The Voice la nchini Uholanzi  limemtangaza Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania kuwa mshindi wa tunzo ya demokrasia mwaka 2014. Tangazo hilo limetolewa na kamati maalumu ya jarida hilo inayohusika na kuandaa tunzo hiyo. Kwa mujibu wa kamati hiyo, Rais Kikwete ameshinda baada ya kuwabwaga washindani wengine wawili ambao majina yao hayakutajwa. Taarifa zaidi zinasema kuwa, Rais Kikwete ameteuliwa kutokana na mchango wake wa kukuza demokrasia ndani ya nchi yake sambamba na kutetea utawala bora barani Afrika. Azma yake ya kuhakikisha Tanzania inapata Katiba mpya ni sababu nyingine iliyochangia ushindi wake.  Rais wa Tanzania anakuwa kiongozi wa pili aliyeko madarakani kushinda tunzo hiyo tangu ilipoanzishwa na anatarajiwa kupokea rasmi tunzo yake mwezi  Septemba mwaka huu kwenye hafla maalumu huko Uholanzi. Mwaka uliopita, Rais wa Sierra Leone, Earnest Bai Koroma ndiye alyetunukiwa tunzo hiyo. Rais wa zamani wa Zambia, Kenneth Kaunda ndiye aliyekuwa mshindi wa tunzo hiyo mwaka 2012.  Mwezi Aprili mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete pia alishinda tunzo nyingine ya kimataifa kuhusiana na masuala ya utawala bora.

0 comments:

Post a Comment