pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Watu 16 wauawa katika mapigano ya Benghazi, Libya

Watu 16 wauawa katika mapigano ya Benghazi, Libya
Watu wasiopungua 16 wamepoteza maisha yao mjini Benghazi Libya kufuatia mapigano kati ya jeshi la nchi hiyo na wanamgambo wanaoipinga serikali. Duru za hospitali na za kijeshi zimetangaza kuwa, wahanga wengi wa mapigano hayo ni wanajeshi. Aidha miongoni mwa waliouawa wapo raia watatu mmoja wao akiwa ni raia wa Misri, ambao walipoteza maisha yao baada ya nyumba yao kushambuliwa na kombora. Taarifa zaidi zinasema kuwa, watu 81 wamejeruhiwa katika mapigano hayo. Mapigano hayo yalizuka jana baada ya wanamgambo hao kushambulia kambo ya jeshi. Mauaji hayo yametokea siku moja tu baada ya watu 47 kuuawa mjini Tripoli kwenye mapigano makali yaliyotokea kati ya makundi ya wanamgambo hasimu wanaopambana nchini Libya. Mapigano hayo yalijiri wakati makundi hayo yalipokuwa yakipambana kwa shabaha ya kutaka kuudhibiti uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tripoli, ulioko umbali wa kilomita 25 kutoka mji mkuu wa nchi hiyo.

0 comments:

Post a Comment