pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Israel yaua shahidi Wapalestina 620 huko Ghaza

Mtoto aliyeuawa shahidi katika hujuma za Israel Ghaza 
Mtoto aliyeuawa shahidi katika hujuma za Israel Ghaza
Idadi ya wahanga wa mashambulizi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika eneo la Ukanda wa Ghaza, imeongezeka na kupindukia watu 620. Kwa mujibu wa habari rasmi zaidi ya watu 40 wameuawa shahidi hii leo katika maeneo tofauti ya ukanda huo hususan katika maeneo ya Hai Zaitun na Beit Hanun. Moja ya wahanga wa jinai hizo za Wazayuni ni mtoto mwenye umri wa miezi minne. Hii ni katika hali ambayo Brigedi ya Izzudin Qassam tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwaangamiza askari 52 wa Kizayuni akiwemo kamanda wa ngazi za juu wa jeshi la Israel, katika mapigano ya ana kwa ana tangu utawala huo pandikizi ulipoanzisha mashambulizi yake katika eneo hilo. Mbali na askari hao 52, wanamapambano hao wa Palestina, wamesambaratisha magari ya deraya yapatayo 36 na vifaru saba. Wakati huo huo Katibu Mkuu wa Mpango wa Ubunifu wa Kitaifa wa Palestina Mustafa Barghuthi amesisitiza kuwa hakutakuwa na usitishaji vita maadamu adui Mzayuni bado anaendelea kuuzingira eneo la Ghaza. Barghuthi ameyasema hayo hii leo na kuongeza kuwa, ni miaka minane sasa wakazi wa ukanda huo wanateseka kwa matatizo mbalimbali na kwamba umewadia wakati wakazi hao waishi kwa heshima na utukufu. Aidha amesema kuwa, utawala haramu wa Kizayuni hauheshimu makubaliano yoyote unayofikia na Wapalestina.

0 comments:

Post a Comment