pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Waziri wa Israel anusurika kombora la muqawama

Waziri wa Israel anusurika kombora la muqawama
Gazeti la Kizayuni la Yedioth Ahronoth limefichua kuwa, Tzipi Livni, Waziri wa Sheria wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel, amenusurika kuangamia baada ya kuanguka karibu yake kombora la wanamapambano wa Kipalestina jana jioni huko katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Kwa mujibu wa gazeti hilo, Livni alikumbwa na wahka mkubwa, licha ya kwamba hata hakujeruhiwa. Livni amenusurika wakati alipokuwa anatembelea moja ya vitongoji vya walowezi wa Kizayuni karibu na Ukanda wa Ghaza. Baada ya tukio hilo, waziri huyo wa sheria wa utawala pandikizi wa Kizayuni aliondoshwa haraka katika eneo hilo na kukatisha kabisa shughuli hiyo. Hii ni katika hali ambayo utawala huo haramu umekiri kuuawa na kujeruhiwa idadi kubwa ya Wazayuni wakiwemo viongozi wandamizi. Muqawama wa Kipalestina umetangaza kuwa utawala huo unaficha ukweli wa mambo kuhusiana na hasara unayopata utawala wa Kizayuni katika vita vinavyoendelea hivi sasa kati ya pande mbili. Kwa mujibu wa wanamapambano wa Kipalestina, wanamapambano hao jana pekee waliwaangamiza askari wa Kizayuni 23 lakini utawala huo umeficha ukweli.

0 comments:

Post a Comment