Fahad Musana, ambaye ni shabiki wa kutupwa wa klabu ya soka ya 
Chelsea, amefariki dunia baada ya mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, 
Frank lampard, kuifungia Manchester City bao la kusawazisha, katika 
pambano lililopigwa jana baina ya timu hizo mbili.
Musana, mwenye umri wa miaka 24, na ambaye alikuwa mcheza kandanda 
la kulipwa nchini Uganda, alikuwa akitizama mechi hiyo iliyovuta hisia 
za mashabiki wengi katika kona mbalimbali za dunia, na alianguka na 
kuzimia mara baada ya Lampard kusawazisha bao, ikiwa ni dakika chache 
sana tangu aingie kutokea benchi, katika dakika za lala salama.
Alithibitishwa kuwa amefariki baada ya kuwasili katika hospitali ya
 kijeshi ya Bombo, na rafiki wa karibu wa marehemu amenukuliwa na vyombo
 vya habari akisema “Jamaa, amekuwa ni shabiki wa kweli wa Chelsea, 
ambaye angeweza kufanya lolote lile kwa ajili ya klabu hiyo. Tulifanya 
naye mazoezi asubuhi ya jumapili, na hata mchana tukala chakula cha 
mchana pamoja, hakika inasikitisha”
Tukio hili la kusikitisha, limethibitishwa na Shirikisho la vyama 
vya soka nchini Uganda (FUFA), ambalo limetoa tamko lake kufuatia mkasa 
huu wa kushtusha.
“FUFA, limekumbwa na mshtuko baada ya kupokea taarifa za kifo cha 
ghafla cha mchezaji wa klabu ya Simba ya Uganda, Misana Fahad, katika 
hospitali ya Bombo. Mwili wa marehemu bado uko hospitalini hapo, na 
taratibu za mazishi zinaandaliwa na taarifa zitatolewa baadae”, sehemu 
ya taarifa ya FUFA imesomeka hivyo.
Hii si mara ya kwanza kwa mashabiki wa soka kufariki kufuatia timu 
wanazozishabikia kushindwa kuibuka na ushindi katika mechi zao. 
Kumbukumbu za hivi karibuni sana kwa ukanda wetu wa Afrika Mashariki na 
Kati, ni za shabiki mwingine wa soka aliyefariki dunia msimu uliopita, 
baada ya timu aliyokuwa akiishabikia ya Manchester United kupoteza moja 
ya mapambano yake, ilipokuwa chini ya kocha David Moyes






0 comments:
Post a Comment