MWENYEKITI
 Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi, ameshinda tuzo ya 
Mwaka ya Mfanyabiashara Bora Afrika (AABLA), kundi la Afrika Mashariki.
Sherehe za tuzo za AABLA, kundi la Afrika Mashariki zilifanyika 
Septemba 20 mjini Nairobi, Kenya na kurushwa hewani moja kwa moja na 
runinga barani Afrika.
Kwa mujibu wa runinga ya masuala ya fedha na biashara Afrika (CNBC 
Africa), ambao ndio waandaji wa sherehe hizo, tuzo hizo za kila mwaka 
zimebuniwa kwa ajili ya kutambua utendaji uliotukuka katika biashara, 
wenye mafanikio makubwa kwenye sekta zao za biashara na vilevile kwenye 
jamii, ambako biashara hizo zinaendeshwa.
Mengi ambaye alikuwa akichuana na wafanyabiashara wengine wanne wa 
ukanda huu wa Afrika Mashariki, mbali ya kushinda tuzo hiyo pia alipata 
tuzo ya mafanikio katika maisha na kusaidia huduma mbalimbali za jamii 
nchini.
Dk. Mengi amekuwa mstari wa mbele katika kuchangia huduma mbalimbali 
za jamii kama vile kwa wasiojiweza, harakati za kupambana na kuondoa 
umasikini, kusaidia vikundi katika kuinua uchumi na mengine.
Tuzo ya mfanyabiashara bora wa kike Afrika, imechukuliwa na Tabitha 
Karanja ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni yake ya Keroche 
Breweries Limited inayotoa ajira kwa zaidi ya watu 300.
Karanja amekuwa akitoa sehemu kubwa ya faida yake kusaidia jamii na kutoa elimu kwa vijana nchini Kenya.
Watanzania wengine waliopata tuzo hizo ni Ofisa Mtendaji wa Helvetic 
Solar Ltd, Patrick Ngowi, (EA Young Business Leader) na Ofisa Mtendaji 
wa Techno Brain Ltd, Manoj Shanker (Entrepreneur of the Year).






0 comments:
Post a Comment