pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Mugabe: Kuchaguliwa AU kumewauma Wamagharibi

Mugabe: Kuchaguliwa AU kumewauma Wamagharibi
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amepuuza wasi wasi wa nchi za Magharibi kutokana na kuchaguliwa kwake katika nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Afrika na kusema kuwa, wasi wasi huo hauna umuhimu wowote kwake. Rais Mugabe ameyasema hayo jana mjini Addis Ababa siku moja baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika. Rais wa Zimbabwe ameongeza kuwa siasa za madola ya Magharibi kuwawekea vikwazo viongozi wa nchi zisizokubaliana na mienendo yao, ni jambo lisilokubalika kama vile ambavyo hazina itibari yoyote. Rais Mugabe amesisitiza kuwa, kama mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, atafanya juhudi kubwa kwa ajili ya kuinua kiwango cha maisha ya Waafrika. Amefafanua kuwa, atatumia uwezo wake wote katika kuhakikisha maamuzi chanya yanapasishwa na Umoja wa Afrika kwa maslahi ya nchi za bara hilo. Ameongeza kuwa, AU itashirikiana na nchi za Ulaya endapo tu nchi hizo zitaamiliana na umoja huo kwa nia njema ya ushirikiano.

0 comments:

Post a Comment