pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran aanza ziara yake A/Mashariki

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran aelekea A/Mashariki
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alasiri ya leo ameelekea Nairobi mji mkuu wa Kenya akiongoza ujumbe wa maafisa kadhaa wa Iran. Katika safari yake huko Kenya, Muhammad Javad Zarif atakutana na kufanya mazungumzo na waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya na maafisa wengine wa nchi hiyo. Pande mbili hizo zitakuwa na mazungumzo yatakayojadili uhusiano wa Iran na Kenya, masuala ya kieneo na kimataifa. Muhammad Javad Zarif pia atazitembelea nchi za Uganda, Burundi na Tanzania. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, safari yake hiyo huko Kenya, Uganda, Burundi na Tanzania inafanyika kuafutia mwaliko kutoka kwa mawaziri wenzake wa nchi hizo.

0 comments:

Post a Comment