pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Miaka 30 Jela kwa Kumlawiti Msichana juu Ya Kaburi

Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu Ally Rashid maarufu Ally Mwizi kifungo cha miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti kwa nguvu makaburini juu ya kaburi msichana (25) jina limehifadhiwa mkazi wa mtaa wa Kotazi Mjini Mpanda.
Hukumu hiyo iliyovuta hisia za watu wengi wa manispaa ya Mpanda ilitolewa jana na hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.
Upande wa mashtaka ulikuwa ukiongozwa na mwanasheria wa serikali wa mkoa wa Katavi Jamila Mziray.
Awali katika kesi hiyo mwendesha mashtaka mwanasheria wa serikali wa mkoa wa Katavi Jamila Mziray alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa Ally Mwizi alitenda kosa hilo Juni 17 mwaka huu majira ya saa mbili usiku huko katika Makaburi ya Kashaulili yalioko katika mtaa wa Kotazi Mjini Mpanda.
Ilidaiwa kuwa mshtakiwa kabla ya kutenda kosa hilo alimfuata msichana huyo ambaye alikuwa ameibiwa vitu vyake vya ndani ya nyumba hivyo Ally Mwizi alimdanganya kuwa yeye anao uwezo wa kumsaidia kuvipata vitu vyake vilivyoibiwa.
Mziray aliiambia mahakama kuwa baada ya msichana huyo kuahidiwa na mshitakiwa kuwa vitu vyake alivyoibiwa vitapatikana ,aliambiwa amlipe ujira Ally Mwizi kiasi cha shilingi 30,000/= ili aende akamwonyeshe vitu vyake alivyoibiwa na alifanya hivyo.
Alieleza kuwa siku hiyo ya tukio mshitakiwa alimpigia simu msichana huyo majira ya saa mbili ili akamuoneshe vitu hivyo alivyoibiwa .
Mziray alisema baada ya kumpigia simu mshitakiwa alikwenda nyumbani kwa msichana huyo na kumchukua na kisha alikwenda naye kwenye makaburi ya Kashaulili kwa lengo la kwenda kumwonesha vitu alivyoibiwa.
“Baada ya kufika makaburini mshitakiwa alimpiga ngwala msichana huyo na kisha kuanza kumlawiti juu ya kaburi huku akimtishia kumuua endapo angepiga kelele”…
“Baada ya kumaliza haja yake mshitakiwa alimwomba dada huyo waende kwenye nyumba ya kulala wageni inayoitwa King Paris ili wakaendelee kufanya mapenzi zaidi kwa kile alichodai kuwa eneo la King Paris panafaa zaidi kufanyia tendo la ndoa kuliko juu ya kaburi”,alieleza Mziray.
Kufuatia kitendo hicho, msichana huyo alipoamua kupiga mayowe ya kuomba msaada na watu walifika kwenye eneo hilo na waliweza kumkamata mshitakiwa .
Akisoma hukumu hiyo hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa aliambia mahakama kuwa kutokana na ushahidi uliotolewa Mahakamani hapo pasipo shaka yoyote mahakama imemwona mshitakiwa Ally Mwizi kuwa amepatikana na hatia ya kifungu cha sheria Namba 154 kidogo cha kwanza ya makosa ya adhabu sura na 16.
Alisema kutokana na kupatikana na kosa hilo mahakama imemuhukumu Ally Mwizi kutumikia kifungo cha miaka 30 jela ili akitoka gerezani awe na tabia njema kwenye jamii ya watu.

0 comments:

Post a Comment