pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Polisi wamsaka diwani akituhumiwa kwa mauaji

 

Anadaiwa baada ya mauaji hayo aliondoka na kundi hilo kwenye gari na hadi sasa hajaonekana anasakwa
Kyerwa. Diwani wa Kata ya Mabila, Wilaya ya Kyerwa,  mkoani Kagera, anatuhumiwa kufanya mauaji  ya Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nyakatete, Danes Damian na Msaidizi wake,  Johnson Damian  wakidaiwa kufungiwa kwenye nyumba yake na kuteswa kabla ya kufariki.
Mauaji hayo  yalitokea Machi 13, mwaka huu baada ya viongozi hao kutekwa  wakiwa shambani na kundi la watu  akiwatuhumu kuhusika na kifo cha mtoto wa diwani huyo, kilichotokea mwaka jana.
Kijana aliyeshuhudia utekaji huo, Kamugisha Damian alidai siku hiyo jioni akiwa na Danes wakichimba viazi, ghafla walivamiwa na kundi la vijana lililoongozwa na diwani ambaye alitoa amri wakamatwe naye akaambiwa alale kifudifudi.
Katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja, watu sita wameuawa kijiji hicho cha Omukagando, mauaji yanayodaiwa kufanywa na kundi linalojiita ‘Hakuna Kulala’.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi  alithibitisha kuwapo kwa mauaji hayo na kwamba,  diwani huyo anasakwa baada ya kutoroka na gari lake akiwa  na baadhi ya vijana anaodaiwa kushirikiana nao.
Alitaja tukio hilo kama la kikatili na juhudi za polisi kumnasa diwani huyo na kundi lake, hazijafanikiwa baada ya kutorokea sehemu isiyojulikana.  Ofisa Mtendaji Kata ya Mabila, Herman Leonard alisema alipigiwa simu na diwani akimtaka afike ofisini kupokea watuhumiwa aliodai anawatafuta muda mrefu.
chanzo mwananchi

0 comments:

Post a Comment