pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

SABABU 10 ZINAZO SABABISHA FOLENI DAR ES SALAAM



ukizungumzia foleni mkazi wa Dar es Salaam atakuelewa haraka sana kuliko mtu mwingine kwa sababu hili ndo tatizo ambalo kila mtu linamgusa jijini, hii ni kwa wote wanaotumia usafiri binfsi (private transport) na wale wanaotumia usafiri wa umma (public transport), katika makala yangu hii nitazungumzia sababu kuu 10 zinazosababisha foleni jijini,

SABABU KUU 10 ZINAZOSABABISHA FOLENI JIJINI DAR ES SALAAM
1. 
    1. UTUNZAJI MBOVU WA MIUNDO MBINU YA BARABARA
Hii inaweza ikaonekana kama si sababu miongoni mwa sababu zinazosababisha foleni jijini, ukizungumzia miundo mbinu ya barabara unaongelea vitu kam, mifuniko ya chemba barabarani, vibao vya kuonesha alama za barabara, madaraja na vyuma vyake, mitaro ya barabarani, pamoja na Macalvat, utanzaji mbovu wa vitu hivi umesababisha foleni kuongezeka, wananchi wamejihusisha na biashara ya vyuma chakavu inayosababisha kuibiwa kwa mifuniko barabarani, pia vyuma vya madaraja, mifuniko ikiibiwa magari lazima yatapungunza speed sehemu yenye shimo kulikwepa hivo kusababisha foleni, pengine magari kutumia njia moja kwa kusubiriana jambo linaloongeza foleni, hii imechangiwa sana na umaskini wa wananchi

2.    UCHONGAJI NA UBUNIFU MBOVU WA BARABARA
Barabara nyingi jijini zimetengenezwa kwa fikra ya kupita magari tu, pegine ilikuwa ni kwa ajili ya magari adogo ya abiria, barabara hizi hazijazingatia watembea kwa miguu, waendesha baskeli na wale watumiaji wa Pikipiki na Bajaj. Utumiaji wa barabara moja kwa matumizi ya watu tofauti unasababisha msongamano mkubwa wa magari barabarani, hii ni kutokana na kile unachoweza kuita upeo mdogo wa mamlaka zilizo husika katika ujenzi wa barabara hizo

3.    BARABARA ZA CHINI YA KIWANGO
Barabara nyingi jijini zina mashimo, hii ni kutokana na utengenezaji wake uliokuwa chini ya kiwango, hali hii inasababisha magari mengi kushindwa kutembea katika mwendo wake uliopangwa, magari mengi yanatembea mwendo wa kawaida sana katika baadhi ya maeneo kutokana na maeneo yale kukumbwa na mashimo ya kupindukia, Mfano barabara ya kwa remy sinza kupitia tandale ni moja ya barabara ambayo ina mashimo mengi

4.   ONGEZEKO LA KUMILIKI MAGARI KWA WATU WA DAR ES SALAAM
Watu wengi wa Dar es Salaam waanamiliki magari kulinganisha na mikoa mingine kitakwimu, magari yanaongezeka lakini bado miundombinu ya barabara haiongezeki hii ina kuwa haiwezi kutengeneza uwiano sawa kati ya magari yaliyopo na barabara za kupit a magari hayo, familia moja inaweza kumiliki magari 3 magari yote hayo yatoke asubuhi, hapohapo familia zaidi ya 100,000 za aina hiyo zifanye kitu hicho hicho kuelekea sehemu moja, hii itapelekea idadi ya magari 300,000 sehemu moja

5.  MCHANGANYIKO WA VYOMBO VYA USAFIRI BARABARANI
Barabara zetu hazijatengwa kutumiwa kwa aina tofauti za vyombo vya usafiri, mchanganyiko katiika matumizi unasababisha sana foleni, mfano unakuta GUTA liko katikati ya magari, mkokoteni humo humo, hii inasababish amagari yashindwe kutembea katika mwendo unaostahili, kwa sababu speed ya  GUTA na ile ya gari ziko tofauti lakini gari linalazimika kutumia speed ileile ya guta kuepusha ajali

6 AJALI
Aajili ni moja kati ya sababu kubwa inayosababish afoleni katika baadhi ya maeneo jijiini, katika takwimu ajali zote za nchini 75% ni zile zilizotokea Dar es Salaam, Pindi itokeapo ajali magari mengi husimama kupisha uuchunguzi wa ajali hiyo barabarani na hata kama ajali hiyo itasogezwa nje kidogo ya barabara lakinin hutumia mda mrefu sana kufanya hivyo kitu ambacho husababish amsongamano mkubwa wa magari

7     UJENZI MBAYA WA VITUO VYA MABASI
Vituo vingi vya mabasi havijajengwa kumudu magari mengi, pia vituo hivi vimeingia sana barabarani, kitendo kinachosababish ausumbufu kwa watu wanaotumia magari binafsi, magari ya abiria yapopaki barabarani sehemu nyingine ya magari hubaki barabarani inayo wazuia watu wengine kuendelea na safari zao, hii husababisha makelele mengi ya honi na kusababisha foleni  kubwa barabarani
Itaendelea ………

0 comments:

Post a Comment